Timu ya Burkina Faso imefunga magoli
mawili ya dakika za mwisho na kupata matokeo ya magoli 2-0 dhidi ya
Tunisia na kutinga nusu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Mchezaji aliyetokea benchi Aristide
Bance alifunga goli la kwanza kwa shuti la chini la mpira wa adhabu
dakika tano tu tangu atokea benchi.
Prejuce Nakoulma aliihakikishia
Burkina Faso ushindi kwa shambulizi la kushtukiza, baada wachezaji
wote wa Tunisia kwenda kushambulia.
Kwa ushindi huo Burkina Faso
itavaana na Morocco ama Misri katika hatua ya nusu fainali ya
michuano hiyo siku ya jumatano.
Prejuce Nakoulma akimzunguka kipa wa Tunisia na kwenda kufunga goli la pili


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni