.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 29 Januari 2017

SADIO MANE AKOSA PENATI, SENEGAL IKITOLEWA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA

Mchezaji wa Liverpool, Sadio Mane, amekosa penati muhimu wakati Cameroon ikiifunga Segegal magoli 5-4 kupitia mikwaju ya penati na kutinga nusu fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Mane,ambaye ni mchezaji ghali wa Afrika kuliko wachezaji wengine penati yake ilizuiliwa na kipa Fabrice Ondoa, huku mchezaji wa Cameroon Vincent Aboubakar akifunga goli la penati la ushindi.

Senegal iliyocheza vizuri katika mchezo huo ilikuwa na nafasi kubwa ya kushinda katika muda wa kawaida, ambapo shuti la Moussa Sow lilipaa juu na kuufanya mchezo huo uliopigwa kwa dakika 120 kuishia bila goli.

Matokeo hayo yanatoa nafuu kwa Liverpool ambayo ambayo imekuwa ikimkosa Mane, huku jana ikipata kipigo cha kushtua cha magoli 2-1 kutoka timu ya Wolverhampton Wanderers katika kombe la FA.
                                    Sadio Mane akiwa amekaa chini akitafakari baada ya kukosa penati 
Wachezaji wa Senegal wakiwa hawaamini kilichotokea baada mchezaji wao tegemeo Sadio Mane kukosa penati

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni