Carl Frampton amepoteza pambano lake
la kwanza la kulipwa kwa kudundwa na Leo Santa Cruz kwa pointi Jijini
Las Vegas katika pambano la mkanda wa WBA uzito unyoya.
Santa Cruz, 28, raia wa Mexico
alistahili matokeo hayo katika pambano hilo, ameahidi kupambana tena
na Frampton kwa mara ta tatu.
Jaji mmoja alisema pambano hilo ni
sare, huku majaji wawili wakimpa Leo Santa Cruz matokeo ya pointi
115-113.
Bondia Carl Frampton akiwa chini baada ya kupigwa ngumi na Leo Santa Cruz
Ngumi ya kushoto ya Leo Santa Cruz ikiwa imemuingia barabara Carl Frampton
Bondia Carl Frampton akimpiga ngumi ya kichwa bondia Leo Santa Cruz




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni