.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 29 Januari 2017

THEO WALCOTT ATUPIA 'HAT TRICK', WAKATI WELBECK AKIREJE KWA KISHINDO

Theo Walcott amefunga magoli matatu 'hat-trick' huku Danny Welbeck akirejea kwa kishindo dimbani tangu Mei 2016 kwa kufunga magoli mawili wakati Arsenal ikiichakaza Southampton kwa magoli 5-0 katika mchezo wa kombe la FA.

Katika mchezo ambao ulichezwa huku timu zote mbili zikiwa zimebadilisha karibu wachezaji wake wengi, kikosi cha Claude Puel kilijikuta kikifundishwa kusakata soka, baada ya kufanikiwa kutinga fainali ya kombe la EFL dhidi ya Liverpool siku ya jumatano.

Welback, aliyerejea dimbani baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu akiuguza goti baada ya kufanyiwa upasuaji, aliifanya Arsenal iongoze kwa kupachika magoli mawili mazuri ndani ya dakika 22 za kwanza na kumtengenezea Walcott goli la tatu.

Arsenal ikicheza huku kocha Arsene Wenger akifuatilia mpira jukwaani baada ya kufungiwa kukaa benchi mechi nne, iliongeza machungu kwa Southampton baada ya mapumziko baada ya kumuingiza Alexis Sanchez na kumsaidia Walcott kufunga magoli mengine mawili.
                            Danny Welbeck akiwa amepiga mpira uliojaa wavuni na kufunga goli 
                                         Mpira uliopigwa na Theo Walcott ukiwa umejaa wavuni 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni