Timu ya Manchester United
imefanikiwa kutinga fainali ya kombe la EFL ambapo itavaana na
Southampton licha ya kufungwa magoli 2-1 na Hull City katika mchezo
wao wa marudio wa nusu fainali hapo jana.
Kikosi cha Jose Mourinho kilikuwa
kinaongoza kwa magoli 2-0 iliyoyapata katika mchezo wao wa awali
kilishuka jana kikiwa kimefanya mabadiliko ya wachezaji watano katika
dimba la KCOM Stadium.
Mchezaji Tom Huddlestone aliwapatiwa
wenyeji goli la kwanza kwa mkwaju wa penati, lakini Paul Pogba
akasawazisha kabla ya Oumar Niasse kufunga goli la pili akiunganisha
pasi ya David Meyer na kusitisha rekodi ya Manchester United
kutofungwa michezo 17.
Paul Pogba akifunga goli pekee la Manchester United katika mchezo huo
Msenegali Oumar Niasse akifunga goli la pili la Hull City



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni