.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 18 Februari 2017

KIMBUGA CHAUWA WAWILI NA KULETA MAAFA JIJINI CALIFORNIA

Watu wawili wamekufa na makumi kuokolewa wakati kimbunga kikubwa kilichoambatana na mvua kikileta maafa kusini mwa California nchini Marekani.

Mwanaume mwenye umri wa miaka 55 amekufa hospitalini baada ya kupigwa na shoti ya waya wa umeme ulioangukiwa na mti Jijini Los Angeles.

Mwanaume mwingine amekufa maji huko Victorville wakati gari lake aina ya Mercedes liliposombwa na kupinduliwa na maji.

Maafisa wa kikosi cha zimamoto wamewaokoa watu saba na mbwa wawili katika eneo la mto Los Angeles.
Askari wa kikosi cha zimamoto wakimuokoa mwanamke mmoja ambaye gari lake limezingirwa na maji
               Lori likiwa limepinduka chini baada ya kusukumwa na upepo mkali wa kimbunga
         Mmoja wa abiria akipanda basi katika kituo ambacho kilikuwa kimefurika maji ya mvua
             Waokoaji wakiwa wamekata sehemu ya mti mkubwa ulioangukia gari na kufunga barabara

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni