.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 22 Februari 2017

MANCHESTER CITY YAPAMBANA NA KUIBUKA NA USHINDI DHIDI YA MONACO

Manchester City imetokea nyuma mara mbili na kupata faida ya magoli mawili katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 5-3 dhidi ya Monaco katika mchezo uliopigwa katika dimba la Etihad.

Katika mchezo huo Raheem Sterling aliipatia Manchester City goli kufuatia kazi nzuri ya Leroy Sane lakini Monaco wakajibu mapigo kupitia kwa Radamel Falcao na kuongeza goli la pili lililofungwa na Kylian Mbappe.

Falcao alishuhudia penati yake ikiokolewa na kipa Willy Caballero dakika chache tu katika kipindi cha pili kabla ya makosa ya kipa wa Monaco, Danijel Subasic, kumpatia nafasi ya kufunga goli Sergio Aguero.

Raia wa Colombian Falcao, ambaye kwa sasa amerejea kwenye kiwango chake baada ya kushindwa kufanya vyema akicheza kwa mkopo Manchester United na Chelsea, alifunga vyema kwa mpira wa kunyanyua juu uliomshinda kipa Caballero.

Aguero ambaye anahisi alinyimwa penati katika kipindi cha kwanza, alisawazisha kwa kufunga goli kabla ya John Jones kuongeza goli la na kisha mchezaji bora katika mechi hiyo Sane akafunga goli la tano.
                                       Raheem Sterling akifunga goli la kwanza katika mchezo huo
                          Radamel Falcao akifunga goli la ufundi la kuubetua mpira kwa juu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni