.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 13 Februari 2017

MFANYAKAZI WA SHAMBANI AJIUWA BAADA YA MUAJIRI WAKE KUTOMLIPA MADAIA YAKE YA MISHAHARA

Mfanyakazi mmoja wa shambani nchini Kenya, amejiuwa baada ya muajiri wake kushindwa kumlipa malimbikizo ya madai ya mishahara yake ya miaka miwili.

Mfanyakazi huyo, Nelson Anyamba, mwenye miaka 38, amejiuwa kwa kujichoma choma kwa kisu baada ya kutolipwa mshahara wake wa shilingi 5,000 ya Kenya kwa mwezi, kwa muda wa miezi 24.

Mke wa marehemu, Phyllis Sariku, amesema muajiri wa mumewe alikuwa anadaiwa kiasi hicho cha sh 120,000 za Kenya lakini alimlipa sh 5,000 tu, na kusema kiasi kingine amekikata kutokana na maziwa ambayo familia yake ilikuwa ikichukua.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni