.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 12 Februari 2017

REAL MADRID YAPAMBANA KIUME KUENDELEA KUONGOZA LA LIGA

Real Madrid imeendelea kuwa kileleni mwa Ligi Kuu ya Hispania La Liga, mbele ya Barcelona, baada ya kupata ushindi dhidi Osasuna katika mchezo ulioshuhudia tukio baya la kuumia mchezaji Tano Bonnin.

Mchezaji huyo beki wa timu hiyo iliyomkiani mwa La Liga alivunjika mguu, wakati akikabiliana na mchezaji Isco wa Real Madrid, katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo.

Cristiano Ronaldo alikuwa wa kwanza kutumbukiza mpira uliompita kipa, Salvatore Sirigu na kuwafanya wageni Real Madrid waongoze kabla ya Sergio Leon kusawazisha goli.

Isco aliuwahi mpira uliokuwa ukizagaa langoni mwa Osasuna na kufunga goli la pili la Real Madrid, na kisha baadaye Lucas Vazquez akafunga goli la tatu katika dakika za mwisho na kufanya matokeo kuwa 3-1.
            Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kufunga goli la kwanza la Real Madrid
             Kiungo Mhispania Isco akifunga goli kwa utulivu baada ya kuunasa mpira uliokuwa ukizagaa langoni mwa Osasuna

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni