.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 12 Februari 2017

SADIO MANE AISADIA LIVERPOOL KUTOKA KATIKA GUNDU LA KUFUNGWA

Sadio Mane ameibeba Liverpool na kuitoa katika kufanya vibaya hivi karibuni baada ya kufunga mara mbili ndani ya muda wa dakika mbili katika kipindi cha kwanza na kuizamisha Tottenham Hotspur kwa magoli 2-0.

Mshambuliaji huyo raia wa Senegal aliifanya timu ya Liverpool kuongoza alipokimbia na kuiwahi krosi ya Georginio Wijnaldum na kupachika goli wavuni katika dakika ya 16 ya mchezo huo.

Mane akaongeza goli la pili sekunde 138 tu baadaye kwa kujipinda na kuachia shuti la karibu kufuatia mpira uliokuwa ukizagaa katika goli la Tottenham, baada ya kipa Hugo Lloris kuzuia michomo ya Adam Lallana na Roberto Firmino.
                      Mshambuliaji Sadio Mane aliyechini akifunga goli la kwanza la Liverpool
                     Sadio Mane akijipinda kufunga goli la pili la Liverpool katika mchezo huo 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni