.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 11 Februari 2017

TRUMP NA WAZIRI ABE WA JAPAN WAELEKEA MAR-A-LAGO KWA MAZUNGUMZO

Rais wa Marekani Donald Trump na mgeni wake Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe wameelekea Mar-a-Lago kwa ajili ya kucheza gofu na kufanya mikutano yao.

Rais Trump ameungana na mkewe Melania Trump, ambaye alikuwa amevalia koti na blauzi nyeusi, suruari nyeupe na mawani ya jua wakati akipanda ndege ya Air Force One.

Binti wa Trump, Ivanka na mumewe Jared Kushner nayo walikwea kwenye ndege ya Air Force One katika safari hiyo.

Waziri Mkuu wa Japan Abe, ambaye aliambatana na mkewe, walipata mlo wa mchana na rais Trump Ikulu, wakati wakijadili ushirikiano wao mpya wa kibiashara. 
Kutoka kushoto Melania Trump, rais Trump, Waziri Mkuu wa Japan Abe na mkewe wakipunga mkono kuaga kuelekea Mar-a-Lago
Rais Trump, mkewe Melania na mgeni wake Shinzo Abe na mkewe wakiwasili Mar-a-Lago
Rais Donald Trump na mgeni wake Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe wakipata mlo wa mchana katika Ikulu ya Marekani

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni