.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 2 Machi 2017

CRISTIANO RONALDO AIOKOA REAL MADRID NA KUGAWANA POINTI NA LAS PLAMAS

Cristiano Ronaldo amefunga magoli mawili katika dakika za mwisho wakati Real Madrid ikitokea nyuma kwa magoli 3-1 na kutoka sare katika mchezo ambao Gareth Bale alitolewa nje dhidi ya Las Palmas katika dimba la Bernabeu.

Isco aliipatia Real Madrid goli la kuongoza katika dakika ya nane, kala ya Tana kusawasisha kwa shuti kali.

Mshambuliaji wa Wales gareth Bale alionyeshwa kadi nyekundu katika kipindi cha pili kwa kumsukuma Jonathan Viera ambaye allifunga kwa mkwaju wa penati baada ya Sergio Ramos kuushika mpira.

Kevin-Prince Boateng aliifunga Real Madrid goli la tatu kabla ya Ronaldo kufunga goli kwa mpira wa penati na kisha baadaye akafunga kwa kichwa na kupelekea kugawana pointi na Las Palmas.
                             Mchezaji raia wa Wales Gareth Bale akionyeshwa kadi nyekundu
             Cristiano Ronaldo akifunga kwa kichwa goli na kufanya matokeo kuwa magoli 3-3

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni