.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 2 Machi 2017

MANCHESTER CITY YATINGA KWA KISHINDO ROBO FAINALI YA KOMBE LA FA

Timu ya Manchester City imetinga robo fainali ya kombe la FA baada ya kupambana kutoka nyuma baada ya kufungwa goli moja na Huddersfield na kuibuka na ushindi wa magoli 5-1.

Katika mchezo huo wa marudio baada ya kutoka sare tasa, Leroy Sane na Pablo Zabaleta walibadili matokeo kwa kufunga magoli na kisha Sergio Aguero kuongeza la tatu kwa mkwaju wa penati.

Aguero tena akatumbukiza golini krosi ya Raheem Sterling na kuandika goli la nne na kisha baadaye Kelechi Iheanacho akafunga la tano katika dakika ya mwisho za mchezo huo.
                             Mchezaji Leroy Sane akifunga goli la kwanza na Manchester City 
                      Kelechi Iheanacho akifunga goli la tano katika dakika ya mwisho ya mchezo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni