.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 2 Machi 2017

TIMU YA BARCELONA YAIFANYIA KITU MBAYA SPORTING GIJON

Timu ya Barcelona imeichakaza Sporting Gijon kwa magoli 6-1 katika mchezo wa Ligi ya Kuu ya Hispania ya La Liga na kukwea pointi moja nyuma ya vinara wa ligi hiyo timu ya Real Madrid.

Katika mchezo huyo wa jana ambapo kocha wao Luis Enrique alitangaza kuachana na timu hiyo katika msimu wa joto, Lionel Messi alifunga goli la kwanza kwa kichwa na Juan Rodriguez ajakijifunga.

Carlos Castro alifunga goli na kufanya matokeo kuwa magoli 2-1, lakini Luis Suarez na Paco Alcacer wakaongeza magoli mengine kabla ya Neymar naye kufunga kwa mkwaju wa adhabu na Ivan Rakitic kukamilisha karamu.
                                 Lionel Messi akiupiga kwa kichwa mpira uliozaa goli la kwanza
                Luis Suarez akiwa amewapiga chenga mabeki hadi kipa na kufunga goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni