.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 25 Machi 2017

DAVID SILVA AFUNGA GOLI KALI WAKATI HISPANIA IKIICHAKAZA ISRAEL

Kiungo David Silva amefunga goli zuri na kuongeza rekodi yake ya kuifungia timu ya taifa lake ya Hispania wakati wakiibuka na ushindi wa magoli 4-1 dhidi ya Israel.

Mchezaji huyo wa Manchester City amefikisha magoli 29 akiwa na Hispania katika michezo 110, baada ya kufunga katika dakika ya 13 ya mchezo.

Magoli mengine ya Hispania katika mchezo huo wa kuwania kufuzu michuano ya kombe la dunia yalifungwa na mshambuliaji nyota wa Chelsea, Diego Costa, Vitolo pamoja na Isco.
                   Mpira uliopigwa kiufundi na David Silva ukimpita kipa na kuelekea wavuni
                      Diego Costa akiupiga mpira kwa kichwa uliozaa goli la tatu la Hispania

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni