.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 22 Machi 2017

HOSPITALI YA MIOT YA INDIA KUENDELEA KISHIRIKIANA NA SERIKALI YA ZANZIBAR

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na ujumbe wake wakitembezwa chumba cha wagonjwa Mahututi { ICU} katika Hospitali ya Kimataifa ya Miot iliyopo Jimbo la Chennai akiwa ziarani Nchini India
Balozi Seif akipata maeklezio ya Kitaamu ndani ya Chumba cha Maaba kwenye Hospitali ya Miot Nchini India. Wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar bibi Asha Ali Abdulla na Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi ambae pia ni Waziri asiye na Wizara Maalum Dr. Sira Ubwa Mamboya
Balozi Seif akimfariji Bwana Ahmed Murdhed wa Chake chake Kisiwani Pemba aliyelazwa kwa kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Miot iliyopo katika Jimnbo la Chennai Nchini India.
Bibi Faida Tajir Ali Mkaazi wa Kisiwandui Mjini Zanzibar akielezea faraja yake kufuatia ujio wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar na Mjumbe wa Mabara la Mapinduzi Dr. Sira Ubwa Mamboya wakimpa pole kwenye Hospitali ya Miot India.
Balozi Seif akibadilishana mawazo na Sheha wa
Shehia ya Maungani Bwana  Ali Kibwana Juma aliyelazwa kwenye Hospitali
ya Miot akipatiwa matibabu

Mzazi wa Mtoto Mgonjwa Hemed Hafidh aliyelazwa
Hospitali ya Miot India Baba Hafidh Hamid Suleiman akiwasilisha salamu
za shukrani kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Balozi Seif
kwa jinsi SMZ inavyowajali wananchi wake kwa kuwagharamia huduma za
matibabu Nchini India.
Mmiliki wa Hospitali ya Kimataifa ya Miot Jimboni Chennai Nchini India Dr. V.A. Mahandazaz akiagana na Makamu wa Pili wa Rais wa Znzibar Balozi Seif mara baada ya kula pamoja chakula cha mchana Hospitalini pake Miot.

Picha na – OMPR – ZNZ.



Uongozi wa Hospitali ya Kimataifa ya Miot katika Jimbo la Chennai
Nchini India umeahidi kuendelea kushirikiana na Zanzibar  katika kuona
Sekta ya Afya inatengamaa ili huduma zinazotolewa kwenye Hospitali
pamoja na Vituo vyote vya  Afya zinawafikia Wananchi  wote wa Visiwa
wa Zanzibar.
Kauli hiyo imetolewa na Mmiliki wa Hospitali hiyo Dr. P.V.A Mahandazaz
 wakati akizungumza na Ujumbe wa Zanzibar unaoongozwa na Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi uliofika Hospitalini
hapo kuwakaguwa Wagonjwa wa Kitanzania wanaogharamiwa  kimatibabu na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 
Dr.Mahandazaz  alisema mkataba uliotiwa saini hivi karibuni kati ya
Uongozi wa Wizara ya Afya ya Zanzibar na Uongozi wa Hospitali hiyo ya
Miot ni mwanzo wa safari ndefu ya matumaini inayoashiria ushirikiano
mwema utakaoleta faraja kwa Wagonjwa wote Kitanzania waopangiwa kupata
huduma za Afya kwenye Taasisi hiyo.
Alisema yapo mambo mengi ambayo Miot imekusudia kuyatekeleza katika
kipindi kifupi kijacho likiwemo suala la kupatiwa mafunzo kwa
Madaktari na baadhi ya wataalamu wa Afya wa Zanzibar lengo likiwa
kuwajengea uwezo wa kutoa huduma za Afya zinazokusudiwa kupatikana
katika kiwango cha Kimataifa.
 
Dr. Mahandazaz alimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar na
Ujumbe wake uliomo Nchini India kwa ziara ya Wiki moja kwamba
Hospitali hiyo itaendelea kuwahudumia Wagonjwa wa Kitanzania wakati
wowote wanapoamuliwa kupelekwa katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kupata
Huduma za Afya.
Naye Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Bibi Asha Ali Abdulla
ameushuruku Uongozi na Madaktari wa Hospitali ya Miot Jimboni Chennai
kwa jitihada wanazochukuwa za kuwapatia huduma za Afya Wagonjwa wa
Kitanzania wanaofikishwa kwenye Hospitali hiyo.

Bibi Asha alisema inaleta faraja na kuona zaidi ya Wagonjwa 171 wa
Zanzibar tayari wameshapatiwa huduma za Afya zikiwemo operesheni za
maradhi mbali mbali baina ya mwaka 2012 hadi 2015.
Alisema katika kupunguza idadi ya wagonjwa na gharama zake za
kupelekwa nje ya Nchi Wananchi wanaopatwa na matatizo makubwa ya
Kiafya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Afya
inaendelea kuimarisha huduma za Afya katika hatua ya kuwa na Hospitali
za Rufaa.
Hata Hivyo Bibi Asha alisema Zanzibar inahitaji kuwa na Madaktari
Wataalamu zaidi ambapo Hospitali ya Miot inaweza kutoa mchango wake
mkubwa wa Taaluma itakayokwenda sambamba na  upatikanaji wa huduma za Afya katika Hospitali hizo za Rufaa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif  na Ujumbe wake alipata
wasaa wa kutembelea Vitengo mbali mbali vya Hospitali hiyo ya Miot ili
kujionea uwajibikaji wa watendaji wake na baadae kukagua baadhi ya
wagonjwa wa Kitanzania waliolazwa kwa ajili ya kupata huduma za afya
ziliwemo operesheni.
 
Akielezea faraja wanayoipata kutokana na huduma zinazotolewa kwenye
Hospitali hiyo Mzazi wa Mgonjwa Hemed Hafidh anayekadiriwa kuwa na
umri wa miaka miwili Baba Hafidh Hemed Suleiman kwa niaba ya wagonjwa
wa Kitanzania ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  kwa moyo
thabiti  inayoonyesha wa kugharamia Matibabu ya Wananchi wake.
 
Baba Hafidh alimthibitishia Balozi Seif  na Ujumbe wake kwamba
Wagonjwa wa Zanzibar hadi sasa ndio pekee wanaogharamiwa  na Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar huduma za Matibabu wakati wanapopekekwa
katika Hospitali hiyo.
 
Alisema Wapo Wagonjwa kadhaa wanaotoka katika baadhi ya Mataifa ya
Afrika kama Madagaska, Somalia, Kenya, Ethiopia, Sudan na hata  Uganda
kwa ajili ya kupatiwa  matibabu Hospitalini hapo lakini wamekuwa
wakijigharamia wenyewe au familia zinazowapeleka.
 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif na Ujumbe wake
atamalizia ziara yake ya Siku Tano katika Mji wa New Delhi kwa
kutembelea Kiwanda cha Matrekta cha Mahindra, kukutana kwa mazungumzo
na Wafanyabiashara pamoja na Wawekezaji wa India.


Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa ili wa Rais wa Zanzibar

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni