Na Felix Mwagara/MOHA
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, amewataka wananchi wa Wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani kuwapa taarifa za matukio ya uhalifu Jeshi la Polisi bila woga wowote ili Jeshi hilo liweze kuwasambaratisha wahalifu katika maeneo hayo.
Masauni alisema Jeshi hilo ili liweze kufanikiwa katika mapambano yake na wahalifu katika maeneo hilo, nguvu ya wananchi inahitajika sana katika utoaji wa taarifa ya matukio hayo.
Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Bungu wilayani Kibiti, Masauni alisema Jeshi lake limejipanga kikamilifu kwa kupambana na wahalifu na litahakikisha wahalifu hao wanakamatwa wote ili wakazi wa maeneo hayo kuendelea kufanya shughuli zao za kuijenga nchi kama kawaida bila wasiwasi wowote.
Aliongeza kuwa, ili jeshi hilo lifanikiwe zaidi katika mapambano hayo linahitaji msaada wa kupata taarifa ya wahalifu hao kwa kuwa baadhi ya wananchi wanawajua wahalifu hao lakini wanaogopa kutoa taarifa kwa polisi wakiwa na wasiwasi wa kuja kuvamiwa endapo ikijulikana.
Masauni aliwahakikishia usalama endapo watatoa ushirikiano kwa Jeshi hilo kwani umakini utakuwepo na hakuna mwalifu atakaye jua kuwa Jeshi hilo limepewa taarifa zozote, kwani kitendo cha kuto kuripoti taarifa ya wahusika hao ni hatari kwa usalama wa wananchi hao kwani huwezi kujua majambazi hayo yanaweza yakaja siku yoyote kuwavamia wananchi hata kama hawakuhusika kutoa taarifa zozote hivyo njia ya busara kushirikiana na polisi ili Jeshi hilo liweze kufanya kazi yake ya kupambana nao na kuleta usalama zaidi.
“Nchi yetu ni ya amani, na Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea kuleta maendeleo kwa wananchi wake, kama mnavyoona viwanda vinajengwa, na pia mnaendelea kufanya shughuli zenu kwa amani kabisa, sasa ili amani hii iweze kudumu, mnatakiwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi pale ambapo mnakuwa na taarifa na wasiwasi na mtu yeyote katika maeneo yenu ambaye hana nia nzuri na usalama wenu,” alisema Masauni.
Alisema Jeshi la Polisi halipaswi kuogopwa na raia mwema, Jeshi hilo ni rafiki kwa kila Mtanzania mwema ambaye ana uzalendo wa dhati na nchi yake, Jeshi ni rafiki ya wananchi, hivyo wananchi wanapaswa kuwa karibu na Jeshi kwa kuwa hao ndio walinzi wa wananchi pamoja na mali zao.
Aidha, Masauni aliwataka wananchi wa maeneo hayo kufuata sheria ili waweze kuishi kwa amani na ushirikiano na endapo watafanya makosa basi jeshi hilo litawakamata wale wote watakaovunja utaratibu mzuri wa kuishi ikiwemo wale wanaoendesha bodaboda bila kofia ngumu.
“Jeshi halionei mtu, na endapo mtaonewa tafadhali nipeni taarifa kwa njia ya simu au mpigieni msaidizi wangu, na pia mnaweza mkawasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ili shida zenu, kero, malalamiko yote ambayo yapo kinyume na sheria wanayoyafanya baadhi ya polisi wetu wasiokuwa waaminifu tuyajue na kuyafanyia kazi kwa dakika chache,” alisema Masauni.
Kabla ya kufunga mkutano huo na kuendelea na ziara yake katika mikoa ya Lindi na Mtwara, Masauni alitoa namba zake za simu ya mkononi kwa wananchi hao pamoja na ya msaidizi wake, pia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani pamoja na wa Wilaya nao walitoa namba zao kwa ajili ya mawasiliano na wananchi hao.
Mwisho/-
NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, amewataka wananchi wa Wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani kuwapa taarifa za matukio ya uhalifu Jeshi la Polisi bila woga wowote ili Jeshi hilo liweze kuwasambaratisha wahalifu katika maeneo hayo.
Masauni alisema Jeshi hilo ili liweze kufanikiwa katika mapambano yake na wahalifu katika maeneo hilo, nguvu ya wananchi inahitajika sana katika utoaji wa taarifa ya matukio hayo.
Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Bungu wilayani Kibiti, Masauni alisema Jeshi lake limejipanga kikamilifu kwa kupambana na wahalifu na litahakikisha wahalifu hao wanakamatwa wote ili wakazi wa maeneo hayo kuendelea kufanya shughuli zao za kuijenga nchi kama kawaida bila wasiwasi wowote.
Aliongeza kuwa, ili jeshi hilo lifanikiwe zaidi katika mapambano hayo linahitaji msaada wa kupata taarifa ya wahalifu hao kwa kuwa baadhi ya wananchi wanawajua wahalifu hao lakini wanaogopa kutoa taarifa kwa polisi wakiwa na wasiwasi wa kuja kuvamiwa endapo ikijulikana.
Masauni aliwahakikishia usalama endapo watatoa ushirikiano kwa Jeshi hilo kwani umakini utakuwepo na hakuna mwalifu atakaye jua kuwa Jeshi hilo limepewa taarifa zozote, kwani kitendo cha kuto kuripoti taarifa ya wahusika hao ni hatari kwa usalama wa wananchi hao kwani huwezi kujua majambazi hayo yanaweza yakaja siku yoyote kuwavamia wananchi hata kama hawakuhusika kutoa taarifa zozote hivyo njia ya busara kushirikiana na polisi ili Jeshi hilo liweze kufanya kazi yake ya kupambana nao na kuleta usalama zaidi.
“Nchi yetu ni ya amani, na Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea kuleta maendeleo kwa wananchi wake, kama mnavyoona viwanda vinajengwa, na pia mnaendelea kufanya shughuli zenu kwa amani kabisa, sasa ili amani hii iweze kudumu, mnatakiwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi pale ambapo mnakuwa na taarifa na wasiwasi na mtu yeyote katika maeneo yenu ambaye hana nia nzuri na usalama wenu,” alisema Masauni.
Alisema Jeshi la Polisi halipaswi kuogopwa na raia mwema, Jeshi hilo ni rafiki kwa kila Mtanzania mwema ambaye ana uzalendo wa dhati na nchi yake, Jeshi ni rafiki ya wananchi, hivyo wananchi wanapaswa kuwa karibu na Jeshi kwa kuwa hao ndio walinzi wa wananchi pamoja na mali zao.
Aidha, Masauni aliwataka wananchi wa maeneo hayo kufuata sheria ili waweze kuishi kwa amani na ushirikiano na endapo watafanya makosa basi jeshi hilo litawakamata wale wote watakaovunja utaratibu mzuri wa kuishi ikiwemo wale wanaoendesha bodaboda bila kofia ngumu.
“Jeshi halionei mtu, na endapo mtaonewa tafadhali nipeni taarifa kwa njia ya simu au mpigieni msaidizi wangu, na pia mnaweza mkawasiliana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, ili shida zenu, kero, malalamiko yote ambayo yapo kinyume na sheria wanayoyafanya baadhi ya polisi wetu wasiokuwa waaminifu tuyajue na kuyafanyia kazi kwa dakika chache,” alisema Masauni.
Kabla ya kufunga mkutano huo na kuendelea na ziara yake katika mikoa ya Lindi na Mtwara, Masauni alitoa namba zake za simu ya mkononi kwa wananchi hao pamoja na ya msaidizi wake, pia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani pamoja na wa Wilaya nao walitoa namba zao kwa ajili ya mawasiliano na wananchi hao.
Mwisho/-
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni