.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 31 Machi 2017

RAIS JACOB ZUMA AMFUKUZA KAZI WAZIRI WAKE WA FEDHA

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amemfukuza kazi waziri wake wa Fedha, Bw. Pravin Gordhan baada ya siku kadhaa za uvumi wa kuchukua uamuzi huo ulioathiri soko na fedha ya nchi hiyo.

Nafasi ya Bw. Gordhan itachukuliwa na Malusi Gigaba imesema taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais Zuma jana.

Mapema wiki hii rais Zuma alimuagiza waziri Gordhan kurudi nchini na kutohudhuria tukio lililokuwa lifanyike Uingereza.

Katika mabadiliko hayo Sfiso Buthelezi atakuwa Naibu Waziri wa Fedha akichukua nafasi ya Mcebisi Jonas.
                                           Kumekuwapo na shinikizo la kumtaka rais Zuma ajiuzulu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni