.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 30 Machi 2017

RUBANI WA NDEGE YA AMERICAN AIRLINES AFARIKI AKIWA KWENYE NDEGE

Rubani wa ndege ya shirika la ndege la American Airlines amefariki dunia wakati ndege aliyokuwa akiiongoza ikitokea Dalllas kwenda Albuquerque, New Mexico.

Ndege hiyo aina ya Boeing 737-800 ilikuwa katika umbali wa maili mbili kabla ya kutua pale rubani alipowasiliana na uwanja wa ndege kuomba msaada wa dharura wa matibabu.

Ndege hiyo ilitua salama, wakati abiria wakikaribia geti la uwanja walipishana na madaktari waliokuwa wakikimbilia kwenye ndege kutoa msaada.

Shirika la ndege la American Airlines limethibitisha kutokea kwa kifo cha rubani wake huyo aliyetambulika kwa jina la William "Mike" Grubbs.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni