Goli la muda wa ziada lililofungwa
na Alexis Sanchez limeipeleka Arsenal katika fainali ya FA kuvaana na
Chelsea baada ya jana kuifunga Manchester City magoli 2-1.
Sanchez aliivusha fainali Arsenal
katika dakika ya 11 ya muda wa ziada baada ya mabeki wa Manchester
City kushindwa kuzuia mpira wa adhabu wa Mesut Ozil.
Arsenal walionekana kupambana kiume
wakitokea nyuma baada ya Sergio Aguero kufunga goli katika dakika ya
62, lakini Alex Oxlade-Chamberlain akasawazisha goli hilo dakika 11
baadaye.
Sergio Aguero akifunga goli la kwanza katika mchezo huo
Alexis Sanchez akifunga goli lililoipeleka Arsenal katika fainali ya FA
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni