.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 24 Aprili 2017

ALEXIS SANCHEZ AIPELEKA ARSENAL FAINALI YA FA


Goli la muda wa ziada lililofungwa na Alexis Sanchez limeipeleka Arsenal katika fainali ya FA kuvaana na Chelsea baada ya jana kuifunga Manchester City magoli 2-1.

Sanchez aliivusha fainali Arsenal katika dakika ya 11 ya muda wa ziada baada ya mabeki wa Manchester City kushindwa kuzuia mpira wa adhabu wa Mesut Ozil.

Arsenal walionekana kupambana kiume wakitokea nyuma baada ya Sergio Aguero kufunga goli katika dakika ya 62, lakini Alex Oxlade-Chamberlain akasawazisha goli hilo dakika 11 baadaye.
                                        Sergio Aguero akifunga goli la kwanza katika mchezo huo 
                     Alexis Sanchez akifunga goli lililoipeleka Arsenal katika fainali ya FA
Sio Mieleka: Olivier Giroud na Vincent Kompany wakianguka chini wakati wakichuana kuwania mpira

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni