Lionel Messi amefunga goli lake la
500 akiwa na Barcelona katika dakika za majeruhi na kuibuka na
ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Real Madrid iliyobakia na wachezaji
kumi katika dimba la Bernabeu.
Kwa ushindi huo umeifanya Barcelona
kufikisha pointi sawa na Real Madrid katika ligi ya La Liga
wakiongoza, lakini Madrid wao wanamchezo mmoja mkononi.
Katika mchezo huo Casemiro alikuwa
wa kwanza kuwafungia wenyeji goli kabla ya Messi kusawazisha na Ivan
Rakitic kuifungia goli la pili Barcelona na kisha Sergio Ramos
alionyeshwa kadi nyekundu.
Mchezaji aliyetokea benchi James
Rodriguez aliifungia Real Madrid goli la kusawazisha lakini Lionel
Messi akafunga goli la tatu katika dakika ya 101.
Casemiro akifunga goli la kwanza katika mchezo huo
Lionel Messi akifunga goli la tatu lililoipa ushindi Barcelona
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni