Mshambuliaji Christian Benteke ameigeuzia kibao
klabu yake ya zamani wakati Crystal Palace ikiifunga Liverpool
katika dimba la Anfield kwa magoli 2-1.
Benteke alifunga magoli mawili ya
Crystal Palace moja katika kila kipindi, wakati kikosi cha Sam
Allardyce kikipambana kutoka nyuma kufungwa goli la mpira wa adhabu
la Philippe Coutinho na kuibuka na ushindi.
Liverpool ilimuuza Benteke kwa
Crystal Palace kwa kitita cha paundi milioni 5, ikiwa ni kiasi cha
chini kuliko walichomununulia mshmabuliaji huyo Mbelgiji, lakini jana
alikuwa mwimba mchungu kwao.
Philippe Coutinho akipiga mpira wa adhabu uliojaa wavuni
Christian Benteke akifunga moja kati ya magoli yake mawili
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni