Wayne Rooney amefunga goli lake la
kwanza tangu mwezi Januari wakati Manchester United ikiendelea
kufukuzia nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa kupata
ushindi dhidi Burnley.
Rooney alianza kikosi cha
kwanza kwa mara ya pili kwa mwaka huu baada ya kocha Jose Mourinho
kufanya mabadiliko nane kutoka kikosi kilichoifunga Anderlecht ligi
ya Uropa.
Kapteni huyo wa Uingereza alianza
vyema na walifanya shambulizi na kupata goli la kwanza kupitia kwa
Anthony Martial na kisha baadaye Rooney alifunga kwa kuupenyeza mpira golini akiwa kwenye
eneo gumu kufunga na kuongeza la pili.
Anthony Martial akifunga goli la kwanza la Manchester United
Wayne Rooney akijipinda na kufunga goli katika eneo gumu kufunga
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni