Lionel Messi amefunga mara mbili
wakati Barcelona ikiendelea kuongoza msimamo katika Ligi ya La Liga
huku ikiichakaza bila huruma timu inayoelekea kushuka daraja ya
Osasuna.
Katika mchezo huo ambao Barcelona
iliibuka na ushindi wa magoli 7-1 Lionel Messi alikuwa wa kwanza
kufunga goli kabla ya Andre Gomes kuongeza la pili.
Roberto Torres aliipatia matumaini
Osasuna kwa kufunga, lakini magoli ya Gomes na Messi tena, kisha
mengine mawili kutoka kwa Paco Alcacer na moja la Mascherano
yaliwanyamazisha.
Lionel Messi akiachia shuti na kufunga goli katika mchezo huo
Paco Alcacer akijipinda na kuifungia goli Barcelona



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni