.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 27 Aprili 2017

REAL MADRID YACHARUKA NA KUIPA KIPIGO KIZITO DEPORTIVO LA CORUNA

Timu ya Real Madrid imezidi kujiimarisha kuelekea kutwaa ubingwa wa Ligi ya La Liga, kwa kupata ushindi wa kishindo wa magoli 6-2 dhidi ya Deportivo la Coruna.

Madrid inayonolewa na Zinedine Zidane, inapointi sawa na vinara Barcelona lakini wanamchezo mmoja mkononi na inaweza kutwaa ubingwa iwapo itashinda michezo yote iliyobakia.

Katika mchezo huo Cristiano Ronaldo alipumzishwa na Gareth Bale akiwa majeruhi, Madrdid ilipata goli lake la kwanza kupitia kwa Alvaro Morata katika dakika sekunde ya 54.

James Rodriguez alifunga magoli mawili likiwemo la kuubetua mpira kiifundi juu ya kipa, pia Lucas Vazquez, Isco na Casemiro walifunga huku Deportivo wakipata magoli kupitia kwa Florin Andone na Joselu.
                                                  Alvaro Morata akiifungia Real Madrid goli la kwanza 
       James Rodriguez akiachia shuti na kufunga moja kati ya magoli mawili aliyoyafunga

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni