Tottenham imeendelea kuipa presha
Chelsea katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza kufuatia
Christian Eriksen kufunga kwa shuti kali na kuibuka na ushindi dhidi
ya Crystal Palace.
Tottenham ilipata wakati mgumu
kupasua ngome iliyona nidhabu kubwa ya Palace katika karibi kipindi
chote cha mchezo huo wa jana ambao ilionekana kama utaishia kwa sare
ya 0-0.
Lakini Eriksen aliachia shuti la
umbali wa yadi 30 lililojaa katika kona ya chini ya goli katika
dakika za mwisho na kuifanya Tottenham kuwa pointi nne nyuma ya
Chelsea.
Christian Eriksen akiachia shuti ambalo lilizaa goli pekee katika mchezo huo
Beki Mamadou Sakho akibebwa kwenye machela baada ya kuumia goti
Katika mcheo mwingine Arsenal
imeendelea kuwania kumaliza katika nafasi nne za juu katika msimamo
wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya Robert Huth kujifunga goli katika
mchezo ulioishia kwa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Leicester City.
Kipa Petr Cech akifanya jitihada za ziada kupangua mpira uliopigwa na Riyad Mahrez





Hakuna maoni :
Chapisha Maoni