Jimbo la Arkansas limewatekelezea
adhabu ya kifo wafungwa wawili kwa siku moja waliohukumiwa adhabu ya
kifo baada ya Mahakama ya Juu kukataa pingamizi lao la dakika za
mwisho.
Wafungwa hao Jack Jones na Marcel
Williams wote walihukumiwa adhabu ya kifo kwa makosa ya ubakaji na
mauaji waliyoyatenda katika miaka ya 1990.
Jimbo la Arkansas limepanga
kutekeleza adhabu ya kifo kwa watuhumiwa nane baada ya kubaini kuwa
dawa ya sindano wanayotumia kuulia inaisha muda wake wa matumizi
mwisho wa wezi huu.
Hii ni mara ya kwanza kutekelezwa
kwa adhabu ya kifo kwa wafungwa wawili katika siku moja tangu kupita
miaka 17 nchini Marekani.
Kitanda maalum kwa ajili ya kutekelezea adhabu ya kifo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni