.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 28 Aprili 2017

MAROUANE FELLAINI ATOLEWA NJE KWA KADI WAKATI MAN U NA MAN CITY ZIKITOKA SARE

Marouane Fellaini ametolewa nje ya uwanja kwa kumpiga kichwa Sergio Aguero wakati timu za Manchester City na Manchester United ambao ni mahasimu wakuu wa Jiji la Manchester wakipambana na kutoka sare tasa katika dimba la Etihad Stadium.

Matokeo hayo yamemuacha kocha Manchester United, Jose Mourinho, akiwa na furaha kwa kufikisha michezo 24 bila ya kufungwa, mafanikio ambayo yamefikiwa licha ya Fellaini kutolewa nje ya uwanja kwa kufanya kitendo hicho cha kizembe.

Mchezaji raia wa Argentina Aguero nusura afunge lakini shuti lake liligonga mwamba huku kocha wao Pep Guardiola akimaliza mchezo huo akiwa na hofu ya kipa wake Claudio Bravo kupata jeraha na kuondolewa kwa kubebwa kwenye machela.
Marouane Fellaini akimwangalia Sergio Aguero akianguka chini baada ya kumpiga kichwa
               Marouane Fellaini akipewa kadi nyekundu kwa kumpiga kichwa Sergio Aguero
        Sergio Aguero akishika kichwa akishindwa kuamini baada ya kukosa goli la wazi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni