.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 29 Aprili 2017

RAIS DKT. MAGUFULI AONDOKA MKOANI DODOMA NA KUELEKEA MKOANI KILIMANJARO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana wakati akielekea kwenye ndege tayari kwa safari yake ya kuelekea mkoani Kilimanjaro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai wakati wakati akielekea kwenye ndege tayari kwa safari ya kuelekea mkoani Kilimanjaro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Dodoma tayari kwa kuondoka na kuelekea mkoani Kilimanjaro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kabla ya kuondoka mkoani Dodoma na kuelekea mkoani Kilimanjaro.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo nchini(TBA) Elius Mwakalinga kabla ya kuondoka mkoani Dodoma na kuelekea mkoani Kilimanjaro.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na watendaji mbalimbali wa Serikali na Chama kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mji wa Dodoma. Wa kwanza kulia Katibu Mkuu wa Wizara wa Fedha Doto James, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa. Kikao hicho pia kiliwahusisha Viongozi wa CDA, Manispaa ya Dodoma pamoja na Spika wa Bunge Job Ndugai.


Mkuu wa mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kabla ya kuondoka kuelekea mkoani Kilimanjaro . PICHA NA IKULU

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni