Wapigakura wanapiga kura leo nchini
Ufaransa kumchagua rais wao ajaye, huku kukiwa na ulinzi mkali
kufuatia shambulizi hatari Jijini Paris siku tatu zilizopita.
Karibu maafisa polisi 50,000 na
wanajeshi 7,000 wamesambazwa katika maeneo mbalimbali nchi nzima ya
Ufaransa kulinda vituo vya kupigia kura.
Wagombea 11 wanawania kuwa rais
ajaye wa taifa hilo, huku wagombea wanaoonekana kutoa ushindani ni
wale wenye kufuata siasa za mrengo wa kulia na mrengo wa kushoto.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni