Mshambuliaji nyota Zlatan
Ibrahimovic anatarajiwa kwenda kutibiwa na daktari bingwa mashuhuri
nchini Marekani, ili kujaribu kumuwezesha kurejea dimbani baada ya
kuumia vibaya kwenye goti.
Ibrahimovic mwenye miaka 35,
atatibiwa na daktari mashuhuri Dk. Freddie H Fu mapema wiki hii,
kutokana na kuchanika vibaya misuli ya kwenye goti baada ya kutua
vibaya wiki iliyopita katika mchezo wa Ligi ya Uropa dhidi ya
Anderlecht.
Timu ya Manchester United
imethibitisha jumamosi taarifa kuhusu kuumia kwa wachezaji wake
misuli akiwemo Ibrahimovic na beki Marcos Rojo, ambao waliumia wote
waliumia katika mchezo huo walioibuka na ushindi wa magoli 2-1.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni