Chelsea ni kama ishakuwa bingwa wa
Ligi Kuu ya Uingereza, baada ya jana kuilaza Middlesbrough kwa magoli
3-0 ushindi ambao unaifanya Boro kushuka daraja.
Katika mchezo huo uliopigwa katika
dimba la Stamford Bridge, Chelsea ilitengeneza nafasi kadhaa na
alikuwa Diego Costa aliyefunga kwa pande la Cesc Fabregas.
Chelsea iliandika goli la pili
kupitia kwa Marcos Alonso aliyefunga kwa mpira uliopita kati kati ya
miguu ya kipa Brad Guzan na Nemanja Matic akafunga goli la tatu.
Kikosi hicho cha kocha Antonio Conte
kinaweza kuwa mabingwa Ijumaa iwapo kitapata ushindi katika mchezo
wao dhidi ya West Bromwich Albion kwenye dimba la The Hawthorns.
Diego Costa akifunga goli la kwanza la Chelsea katika mchezo huo
Marcos Alonso akifunga goli la pili kwa kupenyeza mpira kati kati ya miguu ya kipa



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni