Mabingwa watetezi Leicester City
imejihakikishia kutokushuka daraja katika Ligi Kuu ya Uingereza,
baada ya kupata ushindi wanaostahili wakiwa nyumbani dhidi ya
Watford.
Leicester ilipata uongozi kupitia
kwa Wilfred Ndidi kuachia shuti umbali wa yadi 10, baada ya Hornets
kushindwa kuokoa krosi iliyopigwa na Danny Drinkwater.
Lecester City waligonga mwamba mara
mbili kabla ya Riyad Mahrez kuongeza goli la pili kufuatia makosa ya
Adrian Mariappa na mpira kumpita Heurelho Gomes.
Marc Albrighton aliongeza goli
katika muda wa majeruhi na kufanya matokeo kuwa 3-0, baada ya kunasa
pasi ya Jamie Vardy.
Riyad Mahrez akifunga goli la pili katika mchezo
Marc Albrighton akikamilisha ushindi kwa kufunga goli la tatu



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni