.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 7 Mei 2017

TIMU YA MANCHESTER CITY YAIFUNGA MKONO CRYSTAL PALACE

Manchester City wamejiimarisha katika kuhakikisha wanamaliza katika nafasi nne za juu za Ligi Kuu ya Uingereza kwa kupata ushindi mnono wa magoli 5-0 dhidi ya Crystal Palace na kukwea juu ya Liverpool hadi katika nafasi ya tatu.

Katika mchezo huo David Silva alifunga goli la kwanza ndani ya dakika mbili tu, likiwa goli lililofungwa mapema mno katika msimu huu, lakini baada ya hapo iliwachukua muda mrefu wenyeji Manchester City kuweza kuutawala mchezo huo.

Kikosi cha Pep Guardiola kilijihakikishia kuondoka na pointi zote tatu katika kipindi cha pili baada ya kapteni Vincent Kompany kufunga kupitia krosi ya Kevin de Bruyne, kisha De Bruyne akifunga la tatu, Raheem Sterling akafunga la nne na Nicolas Otamendi akahitimisha karamu.
                     David Silva akiifungia Manchester City goli la kwanza katika mchezo huo
                                 Kapteni Manchester City Vincent Kompany akifunga goli la pili
                       Raheem Sterling akiachia shuti lililojaa wavunia na kuandika goli la nne

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni