.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 6 Mei 2017

MSHAMBULIAJI ZLATAN IBRAHIMOVIC MCHEZAJI WA PILI KWA UTAJIRI ULAYA

Mchezaji wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic, ameingia katika orodha ya wanamichezo matajiri Ulaya akiwa katika nafasi ya pili nyuma ya kinara wa mwaka 2016 Lewis Hamilton.

Ibrahimovic raia wa Sweden ameingizwa kwenye orodha ya wanamichezo tajiri nchini Uingereza baada ya kujiunga na Manchester United Julai, mwaka jana.

Akiwa na utajiri wa paundi milioni 110, Ibrahimovic amempiku mchezaji mwenzake wa timu yao Wayne Rooney anayeshika nafasi ya tatu akiwa na utajiri wa paundi milioni 93.

Dereva wa Formula 1 bingwa wa dunia Muingereza, Lews Hamilton, anaongoza akiwa na utajiri wa paundi milioni 131.
       Dereva wa mbio za langalanga Lewis Hamilton anaongoza kwa utajiri kwa wachezaji Ulaya

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni