.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 6 Mei 2017

WEST HAM YAITIBULIA TOTTENHAM MAHESABU YA KUFUKUZIA UBINGWA

Mbio za Tottenham kuwafukuzia vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza timu ya Chelsea zimepata pigo kufuatia kufungwa goli na Manuel Lanzini lililoipatia West Ham ushindi.

Tottenham wangeweza kupunguza pengo na vinara hao na kubakia tofauti ya pointi moja tu iwapo wangeshinda katika dimba la London Stadium jana, lakini wakajikuta wakilala.

Katika mchezo huo kipa wa wagonga nyundo wa London, Adrian aliokoa kwa ubora wa juu mipira iliyopigwa na Harry Kane na Eric Dier kabla ya Lanzini kufunga.

Kwa matokeo hayo West Ham wameisaidia Chelsea kuukaribia zaidi ubingwa na sasa inahitaji kushinda michezo yake mwili tu ili kutawazwa kuwa mabingwa.
      Manuel Lanzini akiwa ameachia shuti na kufunga goli pekee katika mchezo huo
           Wachezaji wa Tottenham wakiwa wametingwa na mawazo baada ya kufungwa 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni