Mbio za Tottenham kuwafukuzia vinara
wa Ligi Kuu ya Uingereza timu ya Chelsea zimepata pigo kufuatia
kufungwa goli na Manuel Lanzini lililoipatia West Ham ushindi.
Tottenham wangeweza kupunguza pengo
na vinara hao na kubakia tofauti ya pointi moja tu iwapo wangeshinda
katika dimba la London Stadium jana, lakini wakajikuta wakilala.
Katika mchezo huo kipa wa wagonga
nyundo wa London, Adrian aliokoa kwa ubora wa juu mipira iliyopigwa
na Harry Kane na Eric Dier kabla ya Lanzini kufunga.
Kwa matokeo hayo West Ham
wameisaidia Chelsea kuukaribia zaidi ubingwa na sasa inahitaji
kushinda michezo yake mwili tu ili kutawazwa kuwa mabingwa.
Manuel Lanzini akiwa ameachia shuti na kufunga goli pekee katika mchezo huo
Wachezaji wa Tottenham wakiwa wametingwa na mawazo baada ya kufungwa



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni