.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 15 Mei 2017

RONALDO AFUNGA MAWILI; NEYMAR APIGA HAT-TRICK LA LIGA

Cristiano Ronaldo amefunga magoli mawili wakati Real Madrid ikipiga hatua nyingine katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania 'La Liga' kwa kuifunga Sevilla 4-1.

Katika mchezo huo Real walifunga goli la kwanza kupitia kwa Nacho kwa mpira wa adhabu uliotolewa kwa utata kabla ya Ronaldo kuongeza goli la pili.

Stevan Jovetic alichomoa goli moja baada ya mapunziko, lakini Ronaldo akafunga goli safi la tatu na kufikisha magoli 401 akiwa na Real Madrid na Toni Kroos kafunga la nne.
             Cristiano Ronaldo akifunga goli la pili la Real Madrid katika mchezo huo 
Kwa matokeo hayo Real Madrid inabakia katika nafasi ya pili ikiwa na mchezo mmoja mkononi nyumba ya Barcelona iliyoifunga Las Palmas magoli 4-1 wakati Neymar akifunga hat-trick katika mchezo huo.
Mchezaji Mbrazili Neymar akionyesha mchoro wa sura ya mama yake katika kuonyesha mapenzi kwa mama katika siku ya mama hapo jana

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni