.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 1 Mei 2017

SWANSEA YAIZUIA MANCHESTER UNITED KUSOGEA KATIKA NAFASI YA NNE

Mpira wa adhabu uliopigwa kiufundi na Gylfi Sigurdsson umeipatia Swansea pointi muhimu ikihaha kubakia katika Ligi Kuu ya Uingereza na kuharibu hesabu za Manchester United kutinga katika nafasi ya nne.

Sigurdsson alipiga shuti la kuzungusha kutoka umbali wa yadi 30 lililotinga wavuni huku kipa akibaki anauangalia mpira, na kufanya matokeo kuwa 1-1 baada ya awali Wayne Rooney kufungwa kwa mkwaju wa penati.

Kwa matokeo hayo Manchester United imebakia katika nafasi ya tano, pointi moja nyuma ya mahasimu wao Manchester City ambao wanapointi 66 sawa na Liverpool iliyokatika nafasi ya tatu zikiwa zimecheza michezo sawa.
   Wayne Rooney akifunga kiufundi mpira wa penati kwa kumpoteza mahesabu kipa
     Mpira wa adhabu uliopigwa kiufundi na Gylfi Sigurdsson ukielekea kutinga wavuni 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni