.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 1 Mei 2017

TOTTENHAM HAIJAKATA TAMAA YAENDELEA KUIFUKUZIA CHELSEA

Tottenham imejihakikishia kuwa inaendelea kuwa nyuma ya vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza Chelsea kwa tofauti ya pointi nne baada ya kuwafunga wapinzani wao Arsenal kwa magoli 2-0 katika dimba la White Hart Lane.

Ushindi wa Chelsea 3-0 dhidi ya Everton uliipa presha Tottenhma lakini walijibu mapigo kwa staili nao kwa kupata ushindi na kuendelea na kiwango bora, ikilinganishwa na cha Octoba 1960 waliposhinda michezo 13 mfululizo.

Mchezo wao huo dhidi ya Arsenal uliamuliwa na magoli yaliyofungwa na Dele Alli katika dakika ya 55 likiwa ni goli lake la 21 katika msimu huu, na kisha baadaye Harry Kane akafunga goli la pili kwa mkwaju wa penati.
                    Mchezaji nyota kijana Dele Alli akifunga goli la kwanza la Tottenham 
Harry Kane akijipinda na kuachia shuti la mkwaju wa penati aliopiga kiufundi na kufunga goli la pili

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni