Timu ya Manchester City imepata
ushindi mzuri wa magoli 3-1 dhidi ya West Brom na kurejea tena katika
nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza ikiwa imebakiwa na
mchezo mmoja.
Iwapo watapata pointi moja tu katika
mchezo wao wa jumapili dhidi ya Watford itajihakikishia kumaliza
katika nafasi nne za juu katika msimamo na kukata tiketi ya kucheza
Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Manchester City ilipata goli lake la
kwanza kupitia kwa Gabriel Jesus kufuatia mpira ulioanzia kwa Sergio
Aguero aliyempasia Kevin de Bruyne, aliyemlisha Jesus.
Mpira wa Aguero uliookolewa
usimfikie Jesus ulimkuta De Bruyne na kufunga goli la pili naye Yaya
Toure akafunga goli la tatu na Robson-Kanu akafunga goli pekee la
Sunderland.
Gabriel Jesus akiifungia Manchester City goli la kwanza
Yaya Toure akitumbukiza goli la tatu la Manchester City
Robson-Kanu akifunga goli pekee la West Brom katika mchezo huo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni