.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 15 Mei 2017

TOTTENHAM YAAGA DIMBA LA WHITE HART LANE KWA USHINDI

Magoli kutoka kwa Victor Wanyama na Harry Kane yameipatia Tottenham ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Manchester United katika mchezo wao wa mwisho kucheza katika dimba la White Hart Lane.

Tottenham Hostspurs wanampango wa kuwa na uwanja wao mpya, utakaojengwa katika eneo hilo hilo, watakuwa tayari kwa msimu ujao wa 2018-19 wakicheza michezo ya nyumbani katika dimba la Wembley msimu ujao.

Katika mchezo wa jana Wanyama aliipatia Tottenham goli la kwanza kwa mpira wa kichwa katika kipindi cha kwanza kisha Kane akaongeza la pili katika kipindi cha pili kabla ya Wayne Rooney kufunga goli pekee la Manchester United.
                        Victor Wanyama akiruka juu na kufunga goli kwa mpira wa kichwa 
                                                   Harry Kane akifunga goli la pili la Tottenham 
                        Mkongwe Wayne Rooney akifunga goli pekee la Manchester United

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni