.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 7 Mei 2017

WANAFUNZI WAKIKE 82 WALIOTEKWA WAACHIWA NA KUNDI LA BOKO HARAM

Wanamgambo wa kundi la Kiislam la Boko Haram wamewaachia wanafunzi wa kike 82 kati ya 276 waliotekwa kaskazini mashariki mwa Nigeria miaka mitatu iliyopita.

Ofisi ya rais imesema wanafunzi hao wameachiwa katika makubaliano ya kubadilishana na watuhumiwa wa kundi la Boko Haram baada ya mazungumzo.

Wasichana hao watapokelewa na rais wa Nigeria Muhammadu Buhari katika Jiji la Abuja siku ya leo, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa.

Kabla ya kuachiwa kwa wanafunzi hao wa kike, wanafunzi 192 walikuwa bado hawajapatikana tangu walipotekwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni