.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 19 Julai 2017

MAJALIWA ASHIRIKI MAZISHI YA LINAH MWAKYEMBE

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mbeya, Erasto Zambi (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Songwe mkoani mbeya kuhudhuria mazishi ya Linah George Mwakyembe yaliyofanyika Kyela, Julai 19, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo baada ya kuwasili nyumbani kwa Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kushiriki katika mazishi ya mke wa Waziri huyo, Linah George Mwakyembe yaliyofanyika Kyela Julai 19, 2017. Kulia ni mkewe Mary(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Askofu, Rabison Mwakanani wa Kanisa la Evangelical Brotherhood la Mbeya akizungumza katika Ibada ya mazishi ya Linah George Mwakyembe , Mke wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sana na Michezo,Dkt. Harrison Mwakyembe yaliyofanyika Kyela, Julai 19, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (wapili kushoto) wakishiriki katika ibada ya mazishi ya Marehemu, Linah George Mwakyembe, Mke wa Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe katika mazishi yaliyofanyika Kyela Julai 19, 2017. Wengine pichani kutoka kushoto ni Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla, Spika wa Bunge, Job Ndugai, Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson Mwansasu kulia ni Waziri wa Kilimo na Mifugo, Dkt . Charles Tizeba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa dini walioongoza ibada ya mazishi ya Linah George Mwakyembe, mke wa Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe yaliyofanyika Kyela Julai 19,2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu, Linah George Mwakyembe, mke wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe katika mazishi yaliyofanyika Kyela, Julai 19, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dkt. Harisson Mwakyembe pamoja na familia yake wakiwa pamoja na waombolezaji wakati wa Ibada ya ya mazishi ya mkewe, Linah George Mwakyembe yaliyofanyika Kyela, Julai 19, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Mwili wa Linah George Mwakyembe , mke wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe ukiteremshwa kaburini katika mazishi yaoiyofanyika Kyela, Julai 19, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni