.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 24 Julai 2017

POLISI AMPIGA RISASI MWANAMKE BAADA YA SHOO YA WIZKID NAIROBI

Polisi anayetuhumiwa kumpiga risasi na kumjeruhi mwanamke mmoja nje ya Kituo cha Mikutano ya Kimataifa cha Kenyatta (KICC), Jijini Nairobi amekanusha kuhusika na tukio hilo.

Polisi huyo Konstebo Reagan Akoko anatuhumiwa kumpiga risasi na kumjeruhi mwanamke aitwaye Anne Wairimu baada ya tamasha mwanamuziki wa Nigeria Wizkid siku ya jumapili.

Polisi Okoko amesema kulikuwa na gari linazuia wanaotoka kwenye onesho la Wizkid na alipomfuata dereva aliivuta bunduki yake ya aina ya AK 47 na kumsababisha afyatue risasi kimakosa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni