Cristiano Ronaldo ameifungia Real
Madrid moja ya goli zuri kabisa wakati klabu hiyo ikiibuka na ushindi
wa magoli 2-1 dhidi ya Fiorentina na kutwa kombe Santiago Bernabeu.
Katika mchezo huo Real Madrid
ilikuwa ya kwanza kufungwa goli kupitia kwa mchezaji wa Fiorentina
Jordan Veretout.
Ronaldo anayetumikia adhabu katika
La Liga alitoa pande Borja Mayoral aliyefunga goli la kusawazisha, na
kisha baadaye naye kufunga goli la pili kwa shuti kali.
Cristiano Ronaldo akijipinda na kuachia shuti lililoipa ushindi Real Madrid
Wachezaji wa Real Madrid wakinyanyua kombe juu kwa furaha
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni