Mabingwa wa Kombe la EFL, timu ya
Manchester United itaanza kulitetea kombe hilo ikivaana na klabu ya
Burton Albion katika dimba la Old Trafford.
Droo iliyofanyika leo Beijing kwa
matakwa ya wadhamini kinywaji cha Carabao, Liverpool itavaana na
wapinzani wao wa Ligi Kuu ya Uingereza timu ya Leicester City.
Manchester City wao watalazimika
kwenda kuvaana na West Brom, huku timu ya Arsenal ikikutana na timu
ya Doncaster Rovers.
Wadhamini wa Kombe la EFL kinywaji cha kuongeza nguvu cha Carabao
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni