.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 13 Agosti 2017

LUKAKU AANZA KULIPA GHARAMA ZA KUNUNULIWA KWA KUTUPIA MAGOLI MAWILI

Romelu Lukaka amefunga magoli mawili katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya Uingereza akiwa na Manchester United huku nao Anthony Martial na Paul Poga wakifunga goli moja kila mmoja.

Katika mchezo huo uliopigwa katika dimba la Old Traford Lukaku alifunga goli la kwanza katika dakika 33 kwa shuti kali, nyota huyo raia wa Ubelgiji aliongeza goli la pili katika kipindi cha pili kwa kichwa kiunganisha mpira uliopigwa na Henrikh Mkhitaryan.

Mfaransa Anthony Martial alifunga goli la tatu akiingia dimbani kuchukua nafasi ya Marcus Rashford kisha karamu hiyo ya magoli ilihitimishwa na shuti zuri la mbali lililopigwa na Paul Pogba katika dakika ya 90.
                             Romelu Lukaku akifunga goli lake la kwanza katika mchezo huo 
                                      Anthony Martial akifunga goli la tatu la Manchester United
                             Kiungo mshambuliaji Mfaransa Paul Pogba akifunga goli la nne

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni