Naibu Waziri wa Elimu wa Afrika
Kusini Mduduzi Manana amefikishwa mahakamani akikabiliwa na shtaka la
kumshambulia mwanamke kwenye klabu ya usiku.
Naibu waziri huyo ameachiwa kwa
dhamana ya dola 375 baada ya kusomewa shtaka lake, akingojea
uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.
Manana ameomba msamaha kwa kitendo
chake hicho cha aibu, na kusema alichokoza lakini alipaswa pia
kujizuia hasira zake.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni