Bondia Mmarekani Floyd Mayweather
amemuonya mpinzani wake Conor McGregor kuwa kujiamini kwake
hakutamsaidia kitu, huku akionyesha mikwara mizito katika mazoezi
yake.
Mayweather amesema kuwa baada ya
tambo za maneno kwa mwaka sasa yupo tayari kuzidunda na McGregor
katika pambano lao Agosti 26.
Bondia Mayweather ameonyesha uwezo
wake wa kupigana mbele ya vyombo vya habari kwenye gym yake
anayoimiliki.
Bondia Floyd Maywether akijifua mbele ya vyombo vya habari
Bondia Maywether akipiga ngumi kwa mkono mmoja huku mkono mwingine ukiwa umeshikilia glasi yenye kinywaji
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni