Timu ya Barcelona imeibuka na
ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Real Betis ushindi uliochangiwa na
jitihada za nyota wao Lionel Messi katika mechi yao ya kwanza ya La
Liga.
Katika mchezo huo Barcelona walikuwa
wamevalia jezi ambazo zina jina la mji wao mgongoni katika kuomboleza
watu waliouwawa katika tukio la ugaidi.
Barcelona walipata goli lao la
kwanza kupitia kwa Alin Tosca aliyejifunga akijaribu kuzuia krosi ya
Gerard Deulofeu na kisha Sergi Roberto kufunga goli la pili kwa
penati.
Alin Tosca akiangalia mpira aliougonga kimakosa ukimshinda kipa wao na kutinga wavuni
Mchezaji Sergi Roberto akifunga goli la pili kwa mkwaju wa penati
Wakati huo huo mabingwa watetezi
Real Madrid nao wameanza La Liga kwa ushindi wa magoli 3- dhidi ya
Deportivo, huku Gareth Bale, Casemiro na Toni Kroos wakifunga magoli
hayo.
Sergio Ramos akipewa kadi nyekundu na kutolewa uwanjani baada ya kupata kadi mbili za njano katika mchezo huo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni